Tuesday, 2 August 2016

MKUTANO NA WADAU KATIKA MANISPAA YA MOSHI VIJIJINI

 Mkutano na wadau wa afya juu ya program ya hedhi salama katika manispaa ya moshi vijijini
 Wadau wa afya katika wilaya ya Moshi wakisikiliza kwa makini ufafanuzi wa program ya hedhi salama unaotegemewa kuanzishwa katika shule za msingi na sekondari zilizopo moshi vijijini
 Bi Hyasintha Ntuyeko akieleza kwa kina madhumuni ya programu hii ya hedhi salama katika wilaya ya moshi vijijini
 Dokta Wonanji ambaye pia ni mganga mkuu katika wilaya ya moshi vijijini akisikiliza ufafanuzi wa programu hiyo ya hedhi salama unaotarajiwa kuanzishwa katika wilaya yake
Mdau wa afya akiuliza swali la ufafanuzi kwa Bi. Hyasintha Ntuyeko kuhusu programu ya hedhi salama wilayani hapo
 Bi. Hyasintha Ntuyeko ambae pia ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Kasole secrets akiendelea kujibu na kufafanua zaidi jinsi wanavyotarajia kuendesha program hiyo ya hedhi salama katika wilaya ya moshi vijijini
 Mganga mkuu wa wilaya ya moshi vijijini, Daktari Wonanji akitoa tathimini yake kuhusu mradi wa hedhi salama unaotarajiwa kuanza wilayani kwake

 Bi. Hyasintha Ntuyeko akiendelea kufafanua na kuelezea zaidi kwanini mradi wa hedhi salama umelenga kuwahusisha wanafunzi wa masomo ya udaktari kutoka KCMC na kuendelea kuwatoa wasiwasi wadau hawa kwani pia walimu wa afya wa shule zote ambazo zinatarajiwa kufaidika na mradi watapewa mafunzo maalum ambayo yatawasaidia kuendeleza elimu hii ya hedhi salama hata baada ya wao kufunga mradi
 Daktari Wonanji, akiagiza kua mradi wa hedhi salama pia ufikirie kufikia shule nyingi zaidi wilayani moshi vijijini, kwani kuna vijiji ambavyo vimeathirika mno na mabinti hawaendi shule kabisa wakiwa katika hedhi, pia Dr. Wonanji alitoa wito kwa mradi wa hedhi salama kuona ni jinsi gani wataweza kuzifikia shule hizo katika vijiji tajwa hasa katika awamu hii ya kwanza ambapo mradi wa hedhi salama unatarajiwa kutekelezwa
Bi. Hyasintha Ntuyeko akisikiliza kwa makini maoni mbalimbali ya wadau wa afya. Mradi wa hedhi salama katika wilaya ya moshi vijijini utatekelezwa na taasisi mbili yaan Msichana Initiative ambao watatekeleza katika shue za msingi na Kasole secrets co. ltd ambao watatekeleza katika shule za sekondari, taasisi hizi mbili zinapokea ufadhili kutoka ubalozi wa Marekani nchini Tanzania

0 comments: