Wednesday, 31 August 2016

Mkuu wa shule Benignis sekondari aomba mafunzo yawafikie wanafunzi wote shuleni hapo

Sr. Tryphonia Mgando, mkuu wa shule wa sekondari ya Benignis akifungua mahafali ya club ya Pamoja shuleni hapo
Wahitimu 40 wa Pamoja Club wakisimama kwa heshima na kuimba wimbo wa shule wakati wa mahafali ya club ya Pamoja katika shule ya wasichana Benignis
Wanafunzi waalikwa waliokuja kushuhudia wanafunzi wenzao wakihitimu mafunzo ya hedhi salama na ukuaji, wakiimba kwa heshima wimbo wa shule katika mahafali hayo
Wahitimu wa club ya Pamoja wakikabidhi risala yao kwa Mgeni Rasmi, Bi. Hyasintha Ntuyeko ,Mkurugenzi mtendaji wa Kasole Secrets
Wahitimu wakifanya igizo fupi juu ya balehe na changamoto wazipitiazo shuleni
Wahitimu wakiigiza tabia za watoto wa kiume wakifikia balehe na jinsi inavyokua hatari wakikosa washauri sahihi mapema
Sr. Tryphonia Mgando, akipokea cheti cha heshima kwa kuonyesha ushirikiano wa pekee katika kuhakikisha wanafunzi wake wanapatiwa muda wa kutosha kuhudhuria Club
Matroni shule ya sekondari Benignis akipokea cheti cha heshima
Mkuu wa Shule msaidizi, Mwl. Komba akipokea cheti cha heshima
Mwalimu wa taaluma, shule ya sekondari Benignis akipokea cheti cha heshima
Bwana. Revocutus Shigi akipokea cheti cha heshima kwa niaba ya umoja wa wanafunzi wa Udaktari Tanzania (TAMSA)
Wahitimu Pamoja Club, wakiwa katika picture ya Pamoja
Wanafunzi 40 katika shule ya Benignis walifanya mtihani na kufaulu vizuri na leo wamehitimu, tunategemea walimu hawa kua mfano na walimu wa wenzao hapo shuleni waliokosa nafasi ya kujiunga na club
Picha ya Pamoja kati ya wahitimu na jukwaa kuu baada ya kupokea vyeti vyao
Sr. Tryphonia Mgando akitoa shukrani zake za dhati kwa uongozi wa Kasole Secrets kwa kuwaletea program ya Pamoja shuleni kwake na kusaidia mabinti shuleni hapo, Sr. Tryphonia aliwaomba Kasole Secrets kuendelea na program hiyo hapo shuleni kwake ili wanafunzi wengi zaidi wafikiwe

0 comments: