Monday, 8 August 2016

HEDHI SALAMA TRAINING FOR TRAINERS IN MOSHI

  Volunteers wa hedhi salama wakifanya presentation juu ya mchango wa jamii katika kufanikisha hedhi salama kwa watoto wa kike, mjadala huu uliongozwa na Mwl. Yohana, Julius (KCMC), Hariet (KCMC) na Bi. Conjeta Kessy (Afisa Elimu afya na lishe- Moshi Vijijini)
Volunteers wa hedhi salama wakifanya presentation juu ya mila na tamaduni mbalimbali zinazosababisha watoto wa kike washindwe kumudu hedhi salama. Mjadala huu uliongozwa na Mwl. Prisca, Bhavya (KCMC) na Charles (Childreach)
Volunteers wa hedhi salama wakifanya presentation kuhusu njia mbalimbali zinazotumiwa na watoto wa kike katika kujisitiri wakati wa hedhi, mjadala huu uliongozwa na Mwl. Lucy, Angelina (KCMC) na Mwl. Mrema
Dr. Aidat Mugula ambaye pia ni mwalimu wa wakufunzi wa hedhi salama akifafanua kwa kina juu ya hatua mbalimbali za hedhi na mfumo mzima wa uzazi wa mwanamke.

Bi. Rebeca Gyumi, mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Msichana Initiatitive ambao pia ni watekelezaji wa program ya hedhi salama katika shule za msingi akitoa semina jinsi ya kua mbunifu katika kuongoza vikundi vya wanafunzi  mara volunteers hawa watakapoenda kufundisha juu ya hedhi salama katika shule zao.
Bi. Hyasintha Ntuyeko akiendesha semina juu ya mbinu mbalimbali za kufundisha watoto wa kiume kuhusu ukuaji na hedhi salama bila kuwafanya vijana hao kujisikia kudhalilishwa
Wanafunzi wa shule faidika wa mradi wa hedhi salama na wanafunzi wa masomo ya udaktari wakiwa katika group discussion, moja ya mbinu ambazo wakufunzi hawa watapaswa kuzitumia katika shule zao wakifundisha juu ya hedhi salama na ukuaji

Wakufunzi wakiwa katika mijadala ambapo walipatiwa maswali na kuyajadili na baadae kufafanua walichokijadili katika kundi kubwa lenye wakufunzi wote
Wakufunzi wakiandika yale waliyoyajadili katika kikundi chao, tayari kwa kuwasilisha katika kundi kubwa la wakufunzi wote
Dokta Aidat Mugula akitoa muongozo kwa wakufunzi wakati wakijiandaa kumsikiliza Jo Rees, Muuguzi mkongwe kutoka Australia ambae pia ni mtungaji wa muongozo wa mafunzo ya hedhi salama na ukuaji, yanayotumika kufundishia wakufunzi hawa katika warsha hii
Michezo ya Pamoja iliyofanywa na wakufunzi kwa lengo la kuimarisha umoja na kuchangamsha akili na mwili
Bwana Wilson Bigambo, akifundisha wahitimu wenzake mchezo mwingine
Michezo ni sehemu kubwa ya mbinu hodari kabisa katika kuwafundisha watoto wa kike na wakiume juu ya hedhi salama na ukuaji
Jo Rees akijibu maswali mbalimbali yaliyokua yanaulizwa na wakufunzi ni jinsi gani wanaweza kuwahamasisha watoto wakike na wakiume kusoma kwa pamoja juu ya hedhi salama na ukuaji bila kuhisi kudhalilishwa
Moja ya kikundi kikiwasilisha maoni yao katika group kubwa la wakufunzi wote baada ya kujadiliana kama kikundi
Wakufunzi wakipata chakula cha pamoja wakati wa mapumziko
Mazungumzo na kutengeneza mtandao baina ya wakufunzi wakati wa chakula

0 comments: