Thursday, 30 April 2015

MAANDALIZI YA SIKUKUU YA HEDHI DUNIANI NA CTN TV

 Kipindi hiki kilikua live na kilichukua masaa 3 ambapo wananchi  walipiga simu na kutuma meseji, ni kweli jamii yetu inahitaji msaada, changamoto zinazowakuta wanawake wakati wa hedhi zinaathiri jamii nzima, tushirikiane kwa upendo
 Vitabu hivi vimeandaliwa na Kasole Secrets na kuchapishwa kwa msaada wa JHM foundation, vitabu hivi vinatoa ujumbe mhususi kwa jamii nzima ya Tanzania, vikimtaka kila mmoja wetu kusimama katika nafasi yake, kila mmoja abebe jukumu lake ili tuweze kufikia malengo, hatuwezi kufikia malengo kama upande mmoja pekee ndo utabeba jukumu hilo
Mwanahabari Batuli wa CTN akihoji zaidi juu ya nia ya kua na sikukuu ya hedhi duniani, alitaka kusikia zaidi juu ya faida ya siku ya hedhi duniani na baadae kuwapelekea taarifa hizi Watanzania kupitia taarifa ya habari.

0 comments: