Tuesday, 30 August 2016

WANAFUNZI 34 IFAKARA WAHITIMU MAFUNZO JUU YA HEDHI SALAMA NA UKUAJI

Wanafunzi Bravo sekondari wakifurahia vyeti vyao walivyotunukiwa baada ya kuhitimu mafunzo ya hedhi salama na ukuaji yaliyotolewa kwa muda wa wiki 12 shuleni hapo, Mafunzo haya yaliwaweka watoto wakike na wakiume katika club iliyopewa jina la Pamoja, Wanafunzi wa masomo ya udaktari kutoka chuo cha Mtakatifu Francis waliendesha mafunzo haya kwa wiki 12 chini ya usimamizi wa kampuni ya Kasole Secrets

Wahitimu wa Club ya Pamoja wakiimba wimbo katika mahafali yao ya hedhi salama na ukuaji
Wahitimu wa Pamoja Club, wakitoa igizo lao kuhusu hedhi salama na ukuaji, Igizo hili lilionyesha ni kwa kiasi gani mila na tamaduni zinavyoathiri vijana katika balehe
Timu nzima ya jukwaa kuu, ikichukua picture ya pamoja baada ya kumaliza zoezi zima la kugawa vyeti kwa wahitimu wa Pamoja Club
Mwalimu wa taaluma shuleni Bravo, Bwana Ally Msweta akikabidhiwa cheti cha heshima na Mkurugenzi mtendaji wa Kasole Secrets, Bi. Hyasintha Ntuyeko, ikiwa ni shukrani kwa kuonyesha ushirikiano wa pekee katika kuhakikisha wanafunzi wanapata muda wa kutosha katika kujifunza
Matroni Evodia akipokea cheti cha heshima baada ya kuonyesha ushirikiano wa pekee katika kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria mafunzo kwa wakati
Bi. Regina Kway, akipokea cheti cha heshima kwa niaba ya Umoja wa wanafunzi madaktari Tanzania (TAMSA) kwa kukubali kujitoa kwao na kufundisha wanafunzi juu ya hedhisalama na ukuaji
Mwanafunzi Joshua Amani akipokea cheti chake baada ya kuhitimu mafunzo ya hedhi salama na ukuaji kwa majuma 12 shuleni Bravo
Mwanafunzi Mwanahamisi Juma, akipokea cheti chake cha uhitimu baaada ya kuhudhuria mafunzo kwa majuma 12 na kufaulu mtihani
Wahitimu wa Pamoja Club wakifuatilia kwa umakini ujumbe uliokua ukitolewa na daktari Elias kutoka hospitali ya Mt. Fransisco alipofika kwenye mahafali hayo
Daktari Elias, bingwa wa magonjwa ya kina mama kutoka hospitali ya Mt. Francis akiwapongeza wahitimu kwa kufuatilia vyema mafunzo juu ya hedhi salama na ukuaji yaliyotolewa shuleni hapo na kuwaambia kwamba anaamini mafunzo hayo yatawasaidia kujikinga na magonjwa
Mwalimu wa Taaluma shuleni Bravo, Bwana Alli Msweta akitoa tathimini ya uwepo wa Pamoja club shuleni hapo, Bwana Msweta alisema wanafunzi katika Club ya pamoja waliwasukuma kiasi wakaamua kuwajengea watoto wa kike tanuri la kuchomea taulo zilizotumika, Mwalimu Alli alisema pia Club hii imesaidia sana kubadilisha mienendo ya wanafunzi katika utunzaji wa mazingira na hata miili yao wenyewe

0 comments: