Choo hiki ni mali ya taasis moja nyeti sana ya serikali, iliyopo jijini Dar-es-salaam-Posta
Kama unavyoweza kuona hapo, hiki choo kinahifadhi uchafu, unapomwaga maji uchafu unarudi, na si kwamba hakitumiki, kinaendelea kutumika
Huo ni mlango wa kuingilia kwenye hicho choo, ni mlango mzuri sana, ila yaliyopo ndani ni mtihani mkubwa
Hiki choo pia ni mali ya taasisi nyingine kubwa sana, tena ni wadau wakubwa wa mambo muhimu, kipo maeneo ya posta
Huo ndo mlango wao ulivyo, umetengenezwa kwa Aluminium vizuri tuu, lakini ni sawa tu na kusema choo hakina mlango
Unapokua ndani ya hiki choo, hii ndo hali unayokutana nayo, nafikiri hapana mlango kabisa hapa
Muonekano wa vyoo vyote viwili
Muonekano wa vyoo vyote, ni sawa na kusema tuu, hii taasisi haina vyoo.
Swali langu ni kwamba, kama Taasisi muhimu kama hizi, miundombinu ndo hii, je huko vijijini hali ipoje?
Taasisi hizi hazina sababu zozote za kua na vyoo kama hivi... tunapojiandaa kusherehekea sikukuu ya hedhi duniani, tunatarajia mabadiliko kuanzia ngazi ya familia, pia tunatarajia taasisi hizi kufanya marekebisho ya haraka kwenye vyoo vyao..
Ninawatakia maandalizi mema ya sikukuu ya hedhi duniani.
0 comments:
Post a Comment