Thursday, 23 April 2015

WATANZANIA TUNAPOJIANDAA KUSHEHEREKEA SIKUKUU YA HEDHI DUNIANI, EMBU TUJITAHIDI KUKARABATI MIUNDO MBINU YETU




Sioni sababu yeyote ya msingi ya taasisi yoyote kushindwa kurudishia milango ya vyoo pale inapobomoka, sielewi mjenzi wa vyoo hivi alifikiria nini kujenga vyoo bila kuweka mabomba ya maji au kufanya utaratibu wowote ili mtumiaji wa choo hiki aweze kupata maji akiwa ndani ya choo, sababu ya vyoo hivi kua vichafu na vyenye harufu kali kiasi cha watumiaji kuvitumia wakiwa wameziba pua, siielewi pia ni kosa la nani,
Je watumiaji wa kike ambao watajikuta wapo katika mazingira ya namna hii, watavitumiaje vyoo hivi? Je wataendelea kubaki eneo la kazi? Je ufanisi wa kazi wa huyu mama/ binti utakua wa aina gani katika mazingira haya?
Cha kushangaza zaidi vyoo hivi vipo jijini dar-es-salaam, tena katika mitaa inayoaminika wakazi wake wanakipato cha juu ukilinganisha na mitaa mingine
Kama mjini hali ni hii, je huko vijijini....?

0 comments: