Friday, 26 February 2016

WANAFUNZI WAWA WALIMU WA WANAFUNZI WENZAO KUHUSU HEDHI SALAMA NA BALEHE-IFAKARA

 Hili ni juma la 6 kati ya majuma 12 ambayo wanafunzi hawa wanatarajiwa kuhudhuria vipindi hivi vya hedhi salama na balehe, katika hili juma la 6 wanafunzi walifanya karakana ambapo waliwaalika wanafunzi wenzao ambao hawakupata nafasi ya kujiunga kwenye club, na badala yake hawa waliopata nafasi waliweza kuwafundisha wenzao yale yote waliyofundishwa ndani ya majuma 6 na kujibu maswali kwa usahihi kabisa bila uoga wala aibu, hii inaonyesha ni jinsi gani wanafunzi hawa wanavyoweza kua msaada kwa wanafunzi wenzao, ndugu na hata marafiki zao. Hongereni sana wafundishaji wetu wa kujitolea kutoka chuo cha Udaktari cha Mt. Francis-Ifakara






0 comments: