Friday, 12 February 2016

WAKIMBIZI KAMBI YA NYARUGUSU WAPATA FURSA YA KUONGELEA JUU YA HEDHI SALAMA

Mmoja wa wakimbizi kutoka Congo akielezea baadhi ya mila zinazofuatiliwa na jamii kwa mwanamke anapokua hedhi                                   
Bi. Letisia Lyogello, muhamasishaji wa afya kambini  Nyarugusu kutoka shirika la TWESA, akielezea jinsi mtoto wa kike anavyoathirika na mazingira/miundo mbinu mibovu na hivyo kushidwa kujisitiri kabisa anapokua hedhi
Bi. Abilola Angelique ambaye pia ni mkimbizi kutoka Congo akielezea changamoto mbalimbali zinazomkumba mwanamke na binti kambini hapo na hivyo kushindwa kabisa kujisitiri wanapokua hedhi
Bi. Hyasintha Ntuyeko akizungumza na wafanyakazi kutoka mashirika mbalimbali na viongozi wa wakimbizi kambini Nyarugusu wilayani Kasulu kuhusu hedhi salama kua ni swala mtambuka, madhara yake hayaishii kwa mwanamke mtu bali jamii nzima

Bi. Elizabeth Morrissey, kutoka UNHCR akizungumzia umuhimu wa hedhi salama katika nyanja zote

Bwana Elia Sabula kutoka Shirika la Plan International akielezea umuhimu wa kuhusisha wanaume/wavulana ili kuweza kufanikisha hedhi salama katika nyanja zote za kijamii

Bwana George Tibaijuka kutoka UNHCR, akizungumzia juu ya hatua mbalimbali ambazo UNHCR inachukua katika kuhakikisha wanawake na mabinti wanaweza kujisitiri kambini hapo

Dr. Victor Nyange kutoka UNFPA akizungumzia madhara mbalimbali ya kiafya ambayo yanaweza kumkumba mwanamke endapo hata zingatia hedhi salama

Bi. Christina Mwita, kutoka shirika la IRC (International Refugees Committee) akielezea umuhimu wa kua na miundo mbinu yenye kumsitiri mwanake wakati wa hedhi katika vituo vyote vya kukusanyia wakimbizi (entry points)
Bi. Kimberly Height kutoka shirika la TWESA akizungumzia miundo mbinu ya vifaa vya maji na usafi wa mazingira na vifaa mbali mbali vinavyotumika na mwanamke wakati wa hedhi, Bi. Kimberly alieleza kua wanazingatia ujenzi wa vyoo ambavyo vitamsitiri binti/mwanamke wakati wa hedhi
UNHCR, wakionyesha vifaa vipya ambavyo wanatarajia kuanza kuwagawia wanawake na mabinti kwa ajili ya kuweza kujisitiri wakati wa hedhi na kuacha kutoa khanga ambazo walikua wakizigawa kwa wanawake/mabinti kwa matumizi ya hedhi, UNHCR walifafanua kua, wataendelea kutoa khanga kwa wanawake/mabinti kwa nia ya matumizi mbalimbali na si kwa ajili ya hedhi kama ilivyokua awali


Picha ya pamoja na wote waliohudhuria warsha ya hedhi salama kambini Nyarugusu

0 comments: