Tuesday, 8 November 2016

Mganga mkuu wa wilaya Moshi ahadi kuboresha Hedhi Salama wilayani kwake

 Mganga Mkuu wa wilaya ya Moshi- Dr. Wonanji akiongea katika sherehe za kuhitimisha program ya hedhi salama iliyotekelezwa katika shule nne Moshi-vijijini. Program hii ya hedhi salama ilidumu kwa miezi mitatu wilayani hapo ikitekelezwa na mashirika ya Kasole Secrets na Msichana Initiative kwa ufadhili wa ubalozi wa Marekani
Afisa Elimu Afya wa wilaya ya Moshi, Bi. Conjeta Kessy akizungumza  juu ya mikakati endelevu itakayofanya hamasa iliyoletwa na program ya hedhi salama izidi kudumu katika shule nufaika.

 Bi. Angelina Kahangwa, mmoja kati ya wanafunzi wa udaktari ambao walifundisha wanafunzi wa shule za sekondari na msingi wilayani Moshi katika program ya hedhi salama, akielezea changamoto na mafanikio waliyoyapata kwa kipindi chote walichokua wakitekeleza mradi
Bi. Hyasintha Ntuyeko, Mkurugenzi mtendaji wa Kasole Secrets, akiwaaga walimu na wanafunzi katika sherehe za kuhitimisha mradi wa hedhi salama uliokua wa mafanikio makubwa wilayani Moshi

0 comments: