Wanafunzi wa kike kwa wakiume wakishirikiana kwa pamoja kutengeneza pedi ya kufua katika karakana waliyoifanya kama sehemu ya kuhitimisha mafunzo ya Hedhi Salama wilayani Moshi vijijini. Karakana hii ilikaguliwa na mgeni rasmi, Mganga Mkuu wa wilaya ya Moshi vijijini Dr. Vivian Wonanji
Wanafunzi wahitimu wakionyesha ujuzi wao katika kutengeneza pedi za kufua
Kila mmoja alihakikisha anaelekeza watembeleaji na wanafunzi wenzao waliofika kutembelea karakana yao, jinsi ya kutengeneza pedi za kitambaa.
Binti kwa ushujaa kabisa akionesha pedi ya kitambaa aliyoitengeneza
Mganga Mkuu wa wilaya akitembelea karakana ya kutengeneza pedi za vitambaa na kuuliza maswali mbalimbali kwa wahitimu hawa.
Wahitimu wakimuonyesha ndugu mgeni rasmi ambaye pia ni Mganga Mkuu wa wilaya jinsi wanavyoweza kutengeneza mafagio ya kusafishia vyoo kwa kutumia rasilimali zinazopatikana katika mazingira yao. Elimu hii imewatatulia changamoto ya kuacha vyoo vichafu kwa ajili ya ukosekanaji wa mafagio shuleni.
Wahitimu wakionyesha vifaa mbali mbali ambavyo vinaweza kutumika kama dustibini bila kuingia gharama yoyote.
0 comments:
Post a Comment