Kampuni ya Kasole secrets inayoendesha mtandao wa hedhi salama, leo wameendesha mafunzo ya hedhisalama na balehe kwa wanafunzi wanaosomea masomo ya udaktari nchini Tanzania, wanafunzi hawa wanategemewa kwenda kutoa elimu hii katika shule za sekondary hapa nchini kupitia programu maalumu ijulikanayo kama Pamoja Tanzania program. Programu hii ya Pamoja Tanzania inalenga kupeleka Taulo za glory katika mashule za sekondari kwa bei ya chini kabisa, huku ikitoa elimu ya hedhi salama na balehe kwa wanafunzi wote wa kike na wa kiume.
Programu hii ya hedhi salama inafanya kazi pamoja na umoja wa wanafunzi wa vyuo vya udaktari Tanzania, ambao hawa ndio walimu wetu katika mashule, lakini pia muongozo wa ufundishaji unaotumika umeandaliwa na muuguzi Jo Rees kutoka Australia ambaye aliweza kufaulu katika kuutumia muongozo huu vizuri sana katika shule nchini Ethiopia
Hyasintha Ntuyeko, Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Kasole Secrets akiwafungua mafunzo ya hedhi salama na balehe
Dr. Aidat Mugula akitoa mafunzo ya hedhi salama na balehe kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya udaktari Tanzania, ambao wataenda kufundisha elimu hii katika shule za sekondari zilizopo karibu nao
Mdahalo na michango ya agenda kutoka kwa wakufunzi
Wakufunzi wakiwa kwenye makundi wakijadili na kuchora michoro kuonyesha mabadiliko katika mwili wa binti na kijana na ni kwanini mabadiliko haya hutokea
Michezo ni moja kati ya zana muhimu mno katika kufundishia, wakufunzi wakifanya michezo mabalimbali yenye kufundisha kirahisi na kumfanya mwanafunzi aweze kukumbuka
Dinnah Nyirenda na Lilian Benjamin kutoka Hubert Kairuki Medical School walijishindia taulo za Glory baada ya kuweza kulijaza jedwali lenye kuonyesha mabadiliko ya mwili ayapitiayo bnti na kijana, mchezo huu unajulikana kama puberty bingo
0 comments:
Post a Comment