TUVUNJE UKIMYA

Elimu kuhusu Hedhi Salama ni muhimu kwa vijana wote wa kike kwa wakiume.

TUNAO WAJIBU

Jamii nzima inawajibu wa kuhakikisha binti anapatiwa vifaa vyote muhimu ili aweze kujisitiri katika hali ya usalama zaidi na hivyo kuwa huru kushiriki shughuli mbalimbali.

TUSIWAACHE NYUMA

Elimu ya Hedhi Salama itolewe kwa usawa huku ikiwashirikisha kikamilifu vijana wenye ulemavu

TUCHUKUE HATUA

Wadau wa maendeleo, Serikali na taasisi binafsi tunawajibu wa kuchukua hatua kwa kufanya kazi bega kwa bega katika kuhakikisha tunaboresha sera, miundombinu, elimu kuhusu Hedhi Salama na upatikanaji wa vifaa bora na salama vya kujisitiria

Elimu kuhusu Hedhi Salama ni muhimu katika kuboresha:-

  • Umakini na ufaulu mashuleni

  • Afya ya Uzazi

  • Uchumi na kipato

  • Mazingira na miundombinu

  • Uwajibikaji wa wanaume na wavulana

Our Latest Blog

Monday, 10 December 2018

Fida International yaandaa mafunzo ya Hedhi Salama kwa mabalozi wa Afrika Mashariki